Header Ads Widget

AKINA MAMA WANAONYONYESHA KAHAMA WASISITIZWA KUFUATA USHAURI WA WATAALAM JUU YA UNYONYESHAJI SAHIHI

Akinamama wa kata ya Mwendakulima halmashauri ya mji wa Kahama wanaonyonyesha watoto chini ya umri wa miezi sita wakiwa na zawadi walizopewa na shirika la SHDEPHA+ kupitia maradi wa Tulonge Afya Naweza .

Na  Patrick Mabula-Kahama

Mratibu wa Huduma za Afya Uzazi na Mtoto Halmashauri ya Mji Kahama, Carolyne Marcel amewataka akinamama wanapopata ujauzito kuzingatia elimu ya afya wanayopewa na wataalamu wa afya ili waweze kujifungua salama. 

Akizungumza katika tamasha la  akinamama wanaonyonyesha  watoto walio na chini ya miezi sita wa kata ya Mwendakulima la kutoa elimu kuhusu faida ya kumyonyesha mtoto maziwa ya mama pale anapojifungua  hadi miezi sita  kunavyomsaidia kuwa na afya nzuri ya akili na mwili.

Marcel aliwataka wakinamama wanapopata ujauzito kwanza kuwahi mapema hospitari , kituo cha afya na zahanati na kufaata elimu wanayopewa na wataalamu wa afya na kuacha kufata ushauri wa mitaani unawaosababishia kuweza kupata matatizo wakati wa kujifungua .

Amewataka akinamama kuacha mila na destuli potofu ya kutumia  dawa  za miti shamba wanapokuwa wajawazito  na wanapojifungua wasiwapatie watoto kwa sababu  zimekuwa zikiwasababishia matatizo mbalimbali ya kiafya bali wafaate elimu wanayopewa na wataalamu wa afya na wahudumu wa afya ngazi ya jamii. 

Balozi wa mradi wa Naweza, Zuwena Mohamed maarufu kwa jina la Shilole alisema suala la akinamama kuwanyonyesha watoto wanapojifungua ni la lazima  kama tunavyotakiwa na wataalamu wa afya ili mtoto kumuepusha  kuwa  na utindio wa ubongo unaotokana na sababu ya kutonyonyeshwa ipasavyo  maziwa ya mama.

Akitoa elimu hiyo katika tamasha lililokuwa limeandaliwa na shirika la SHDEPHA+ katika mradi wake wa “ Tulonge Afya Twaweza “ unaohusu kutoa elimu ya afya ya mama na mtoto na umuhimu wa kuwayonyesha watoto  maziwa ya mama anapojifungua tu hadi miezi sita kunavyoweza kusaidia kukuwa vizuri kiakili na kimwili. 

 Kaimu mratibu wa elimu ya afya kwa umma ngazi ya jamii  wa halmashauri ya mji wa Kahama  , Vestina Mutakyahwa kifudisha elimu ya kunyonyesha watoto  alisema mtoto anapozaliwa tu anatakiwa anyonyeshwe maziwa ya mama pekee hadi miezi sita na asipewe  rishe ya aina yoyote kunamfanya akue vizuri kiakili na kimwili. 

Shirika la SHIDEPHA+ linalotekeleza mradi wa TULONGE AFYA TWAWEZA  unaohusu kutoa elimu kwa akinamama  wanaonyonyesha watoto kuanzia  wanapojifungua hadi miezi sita bila kuwapatia rishe yoyote ili waweze kukua vizuri kiakili na kimwili pamoja na kutoa elimu ya afya ya mama na mtoto na matumizi sahihi ya chadarua katika kupambana na ugonjwa wa maralia.

Balozi wa mradi wa USAID Tulonge Afya , Zuwena Mohamed (Shilole) akiwasisitiza akinamama wenye watoto chini ya umri miezi umuhimu wa kunyonyesha mtoto maziwa ya mama kuanzia pale anapozaliwa hadi miezi sita bila kumpatia rishe ya aina yoyote kumuepusha kuwa na utindio wa ubongo.
Mratibu wa huduma za afya ya uzazi na mtoto , halmashauri ya mji wa Kahama Carolyne Marcel akiongea katika tamasha la kutoa elimu ya umuhimu wa kunyonyesha watoto maziwa ya mama anapozaliwa hadi miezi sita , wa kwanza kushoto ni Meneja mwandamizi mradi wa USAID Tulonge afya ,Doris Chalambo , Zuwena Shilole maarufu Shishi Baby , na kulia mwisho mratibu wa afya ya uzazi na mtoto Vestina Mutakyahwa.
Balozi wa Mradi wa USAID wa Tulonge Afya , Shilole maarufu Shishi Baby akiingia kwenye tamasha la kutoa elimu ya afya ya uzazi kunyonyesha watoto chini ya miezi sita.



Post a Comment

0 Comments