Header Ads Widget

B DOZEN: RUGE ANGEKUWA HAI NISINGEONDOKA CLOUDS


 Hamis Mandi 'B Dozen'

Mtangazaji wa Efm na TVE @bdozen amefunguka na kuweka wazi kilichomtoa katika kituo chake cha mwanzo cha habari ambacho ni Clouds Fm.

Akiongea katika mahojiano na kituo chake cha kazi cha sasa TVE ambacho kinasimamiwa na @jonijooo amesema kuwa kuna mambo hayapo sawa ndio maana ameondoka Clouds Fm na huenda marehemu Ruge angekuwepo huenda asingeondoka.

Mbali na hilo @bdozen amezungumzia kuhusu muda ambao CEO wa TVE na EFM @majizzo Kumuomba aondoke Clouds Fm na kusema ametumia miaka mitano kumuomba aondoke Clouds.