Header Ads Widget

PROFESA KABUDI AITAKA OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA(NPS) KUONGEZA KASI YA USIMAMIZI WA MAZINGIRA.

 Waziri wa Katiba na Sheria (Kushoto) Mh.Profesa Palamagamba Kabudi akifungua jengo la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti Mkoani Mara lililoko katika Mji Mdogo wa Mugumu

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe.Profesa Palamagamba Kabudi amesema umefika,wakati sasa wa  Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kuongeza kasi ya kusimamia makosa ya uharibifu wa mazingira kwa ukubwa wake badala ya kazi hizo kufanywa na Baraza la Taifa la Usimamizi na Uhifadhi wa Mazingira ( NEMC) pekee kwakuwa uharibifu wa mazingira ni kosa ni uhujumu uchumi.

Mazingira yetu yanazidi kuharibiwa sana, kuharibu mazingira ni kosa la jinai. Tunakata miti bila huruma. Umefika wakati sasa jukumu la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka katika kusimamia na kutunza mazingira lionekane wazi ili watu wajue kuwa kuharibu mazingira ni kosa la jinai na ni uhujumu uchumi.

Mhe. Kabudi ameyasema hayo katika hafla ya ufunguzi wa jengo la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka wilaya ya Serengeti zilizofanyika mjini Mugumu leo tarehe 21 Septemba, 2021 ambapo alisema sasa kuna umuhimu wa kuipitia  Sheria kuu “Penal Code” ili kuhakikisha baadhi ya makosa yanayohusiana na uharibifu wa mazingira na maliasili yanaingizwa.

Alisema uzinduzi wa jengo la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka wilaya ya Serengeti litasaidia kusogezwa kwa karibu kwa  huduma za mashtaka kwa wananchi pamoja na kuipunguzia serikali gharama za uendeshaji kesi na pia itasaidia kupambana na ujangili katika wilaya ya Serengeti.

Mhe. Kabudi  alisema uhifadhi wa  maliasili za nchi yetu unahitaji ukali wa sheria ili kudhibiti vitendo viovu na kutaka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kuyachukulia kwa uzito makosa hayo kwa kuwa yanahujumu uchumi ambapo alitaka maeneo yote yenye maliasili kuwa na Mawakili wa Serikali ili kupambana na makosa ya uharibifu wa mazingira.

Aidha, Mhe. Kabudi alitumia fursa hiyo kuipongeza Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kwa hatua ya kupata ofisi na wadau wote waliohisani na kuhakikisha kuwa jengo la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka linajengwa.

Naye Mkurugenzi wa Mashtaka Ndg. Slyvester Mwakitalu alisema uwepo wa jengo la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka wilayani Serengeti utasaidia kuboresha utendaji kazi na kuongeza kasi ya utendaji kwakuwa mazingira ya utendaji kazi utakuwa umeboreshwa.

Alisema ujenzi wa Jengo la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka wilaya ya Serengeti ni jambo la kujivunia kwakuwa ni jengo la kwanza kujengwa tangu kuanzishwa kwa Ofisi yaTaifa ya Mashtaka mnamo mwezi Februari 2018. Aidha. Aliwashuru wadau wa Makampuni ya GRUMET kwa kufadhili ujenzi wa jengo hilo na kuwaomba wadau wengine pia kujitokeza kufanya hivyo wanapoombwa kuhisani ujenzi.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Serengeti Mhe. Vincent Mashinji akizungumza katika hafla hiyo alisema uwepo wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka wilaya ya Serengeti utasaidia kuboresha huduma na utaipunguzia serikali gharama za uendeshaji wa kesi na upelelezi ambapo aliahidi kuongeza ushirikiano katika utendaji wa kazi.

Aidha, Mhe. Mashinji aliwataka wakazi wa Serengeti kutii sheria bila shuruti na kuitumia ofisi hiyo kwa kutoa ushirikiano mzuri pale wanapohitajika kutoa ushahidi hali ambayo itapelekea kesi kuisha kwa wakati.Mwonekano wa  mbele wa  Jengo la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya  ya  Serengeti Mjini Mugumu Mkoani Mara 

Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba  Kabudi akikata utepe  kuashiria Ufunguzi wa Jengo la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Mugumu-Serengeti Mkoani Mara.

Baadhi ya Viongozi wakeindelea kufautailia Burudani mbalimbali zilizokuwa zikiendele wakati wa Ufunguzi wa Jengo la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilayani Serengeti Mkoani Mara.

Baadhi ya wakazi wa Serengeti wakiedelea kufuatilia hotuba za Viongozi 

Viongozi mbalimbali wakiendelea kufautilia na kutazama burudani wakati wa ufunguzi wa jengo la Ofisi ya Taifa ya Mashataka Seregenti Mara

Viongozi mbalimbali wakiendelea kufuatilia na kutazama burudani wakati wa ufunguzi wa jengo la Ofisi ya Taifa ya Mashataka Seregenti Mara


Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba  Kabudi akitoa zawadi wa wacheza ngoma  wakati wa ufunguzi wa Jengo la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti.

Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba  Kabudi akitoa tuzo ya  zawadi  kwa Mkurugenzi Mkuu wa Grumet Fund Bw. Noel Mbise ikiwa ni sehemu ya kkutambua mchango wao kwenye ujenzi wa jengo hilo wakati wa ufunguzi wa Jengo la Ofisi ya Taifa ya Mashtaka Wilaya ya Serengeti. 


 

Post a Comment

0 Comments