Header Ads Widget

DPP MWAKITALU AHITIMISHA ZIARA KATIKA MAGEREZA YA UKONGA,KEKO NA SEGEREA AHAIDI KUPELEKA MAHAKAMANI KESI ZENYE USHAHIDI.

 Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Sylvester Mwakitalu akipokea Maelezo kutoka kwa Mkuu wa Gereza la Mahabusu Segerea Mrakibu Mwandamizi wa Magereza(SSP)Daniel Mwakyoma wakati  alipotembelea Gereza hilo Juni 13,2021.

Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP) Sylvester Mwakitalu amehitimisha ziara yake ya kutembelea  na kukagua hali ya Magereza ya Mkoa wa  Dar es Salaam baada ya kutembelea na kuzungumza na Mahabusu pamoja na wafungwa walioko katika magereza yote matatu ya mkoa huo.

Akizungumza mara baada ya kujionea hali ilivyo katika Magereza hayo, baada ya kuhitimisha ziara kwa kutembelea Gereza la Mahabusu Segerea  DPP Mwakitalu  amesema Changamoto alizoziona ndani ya magereza hayo zitamsadia katika kufanya maamuzi na kuboreha utendaji kazi wa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka.

DPP Mwakitalu alisema changamoto zilizowasilishwa na baadhi ya mahabusu walioko gereza la Segerea ambazo  hazipo ndani ya uwezo wa Ofisi ya Mashtaka atakahikikisha anazifikisha kwa wahusika ili ziweze kutafutiwa ufumbuzi ambapo amesema maeneo yanayohitaji suluhisho la pamoja atahakikisha anakaa na wadau ili kutafuta suluhisho la pamoja.

“Kwa changamoto ambazo ziko chini ya ofisi yangu, nitazifanyia kazi kwa  haraka kadri iwezekanavyo ili haki  iweze kutendeka,haya mengine  ambayo yako nje ya Ofisi yangu nitawashirikisha wadau wakiwemo mahakama, wapelelezi na wachunguzi ili tuwe na suluhu ya pamoja”Alisema DPP Mwakitalu

Aidha, DPP Mwakitalu akizugumzia chagamoto ya kuchelewa kwa upelelezi wa mashauri mbalimbali alisema kuwa wapelelezi wanaoshugulikia kesi ni wadau wake wa karibu  kwani bila uwepo wao yeye hawezi kufanya kazi hivyo ameahidi kukaa kwa pamoja  ili kesi zilizoko mahakamani ambazo upelelezi wake haujakamalika uweze kufika mwisho.

Alisema  Ofisi ya Taifa ya Mashtaka katika kutekeleza majukumu yake itaendelea kufanya kazi zake kwa kutenda haki.

Mwakitalu alisema kuwa kwa sasa Ofisi yake kwa pamoja na watendaji wataanza kazi ya kupitia upya majalada ya kesi ili kubaini kama yana ushahidi wa kutosha kesi ziendelee na kama ushahidi wake ni hafifu  atayafanyia maamuzi.

“Naomba  niwaeleze changamoto hizi na ushauri wenu nimeupokea kwa sasa hatua  tulizonazo ni kupitia upya majalada ya kesi ili kuona lipi linafaa kuendlea a lipi linafaa kufanyiwa maamuzi upya”alisema DPP Mwakitalu

Katika hatua nyingine DPP alisema kuwa Ofisi yake kwa sasa  itahikikisha inapeleka kesi mahakamani zenye ushahidi kamili na zile ambazo bado hazijapata Ushaihidi kamili hazitafikishwa Mahakamani ili  kuondoa changamoto ya Msongamano Magerezani .

Kuhusiana na suala la utoaji wa vibali vya kesi DPP Mwakitalu alisema kuwa atahakikisha vibali vya Kesi(Concert)  ambazo zimekwama kutokana na kukosa kibali hicho atahakikisha  vibali hivyo vinatolewa ili kesi ziweze kuendelea.

Aidha, DPP Mwakitalu ametembelea magareza ya Keko,Segerea na Gereza Kuu Ukonga ambapo alisema kuwa huo ni Mwendelezo wa ziara zake za kutembelea na kukagua hali ya magereza hapa nchini, kusikiliza  kero na changamoto za wafungwa na mahabusu ili Ofisi yake iweze kuzitafutia Suluhu

Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Sylvester Mwakitalu akiwasili katika gereza la Mahabusu Segerea na kupokelewa na mkuu wa gereza hilo Mrakibu Mwandamizi wa Magereza Daniel Mwakyoma Mapema juni 13,2021.Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Sylvester Mwakitalu(Kushoto)akisalimiana na Mkuu wa Gereza la Mahabusu wanawake Segerea Mrakibu wa Magereza Iyunge Saganda (wa pili kutoka kushoto) wakati wa ziara ya kutembelea na kusikiliza changamoto za Mahabusu .

Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Sylvester Mwakitalu akisalimiana na baadhi ya maafisa wa magereza katika gereza la Mahabusu Segerea Mkoani Dar es salaam wakati wa ziara yake.Mkuu wa Gereza la Mahabusu Segerea Mrakibu Mwandamizi wa Magereza(SSP)Daniel Mwakyoma  akiwaongoza Viongozi kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka wakiongozwa na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP)Sylvester Mwakitalu kuelekea Gereza la  Mahabusu wanaume.

  

Post a Comment

0 Comments