Header Ads Widget

ICS YAADHIMISHA SIKU YA MAMA DUNIANI KWA KUTOA ELIMU, BUKENE SHINYANGA.

Mkurugenzi wa Shirika lisilo la Kiserikali la  (ICS)Kudely Sokoine akizungumza na watoto katika Kijiji cha Bukene Kata ya Bukene halmashauri ya wilaya ya Shinyanga ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya mama Duniani.

Tanzania leo imeungana na Mataifa mengine Duniani kuadhimisha siku ya Mama ambapo Shirika  lisilo la Kiserikali  la  Wekeza kwa Watoto na Jamii (ICS) limeadhimisha kwa namna tofauti kwa kutoa elimu kwa jamii juu ya kuthamini mchango wa Mama.

Elimu hiyo imetolewa katika Kijiji na kata ya Bukene Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga ambapo Mkurugenzi wa Shirika la(ICS) Bw. Kudely Sokoine ameitaka jamii kujenga tabia ya kutambua mchango wa mama kwenye malezi na makuzi ya familia yoyote.

Kudely amesema ili jamii ijengwe katika uelewa mkubwa wa kuona thamani ya Mama lazima ianzie ngazi ya familia, watoto wakiwa wangali wadogo wajengewe uwezo wa kutambua  thamani ya  mama ambaye ana jukumu kubwa katika familia.

Akizungumza na Shinyanga blog mmoja wa watoto Agape Evaliste amesema kuwa kuna umuhimu wa kumtunza mama pale anapokuwa amefanya kazi nzuri na inayoonekana kwa  jamii hupaswa kupongezwa  tabia ambayo hupaswa kujegwa wakiwa wadogo.

kwa upande wao baadhi ya fulsa ya kueleza nafasi ya  teknolojia ya mawasiliano katika kuimarisha mawasiliano, Elias Moses amesema kuwa ujio wa teknolojia ya habari na mawasiliano katika maeneo yao hususani simu na Luninga  imechangia kwa kiwango kikubwa kufikia maendeleo na kukuza mahusiano katika jamii,sambamba na kufikisha ujumbe kwa haraka.

Moses ameongeza kwa kusema kuwa  maeneo ya vijijini yalisahaulika kwa muda hivyo ujio wa simu na  luninga umewafanya na wao kuwa sehemu ya jamii za kitanzania na kuendana na dunia ya mabadiliko ya sayansi na teknolojia sanjali  na kukuza ucumi wao kwa kuwa simu imekuwa ikitumika katika kuwasiliana na wateja wao.

Kauli ya Moses inaungwa mkono na Paulo Mmdege ambaye amesema kuwa mawasiliano ya simu kwake yamekuwa msaada mkubwa wa kuwasiliana na ndugu zake walioko mbali hali inayochangia kutatua changamoto za familia kwa wakati.

Kwa upande wake Eva Joseph amesema kuwa ujio wa mawasiliao ya simu kumesababisha migogoro mingi   kwa baadhi ya familia kutokana na wengi wa wanaume kutumia muda mwingi kuchati, badala ya kuzungumza na familia zao hali  inayoleta utengano kwenye maisha ya kila siku.

Naye Maria Mathayo ameongeza kuwa kutokana na mila na desturi zao, wanaume wengi kwa sasa wanatumia muda wao mwingi kwenye simu kuliko kujishulisha na uzalishaji mali, na kuwaacha wanawake  kuwa wazalishaji wakuu ambao hawewezi kuzalisha chakula cha kukidhi jamii au familia nzima.

Akihitimisha mjadala wa  elimu juu ya  mapokeo ya teknolojia kwa jamii, Mkurugenzi wa Shirika la(ICS) Bw Kudely Sokoine amesema kuwa katika utafiti wao mdogo wamebaini kuwa ujio wa teknolojia maeneo ya vijijini umechangia kwa kiwango kikubwa  mmonyonyoko wa maadili kwenye jamii.

Aidha Kudely amesema licha ya maadili kummonyonyoka pia watoto wengi kwa sasa hutumia muda huo kuangalia simu na tv badaa ya kusoma ili kuandaa maisha yao ya baadaye.

Siku ya Mama uadhimishwa kila ifikapo May 9,  ya kila mwaka ikiwa ni kukumbuka na kuthamini mchango wa mama kwenye jamii kwa kuzinagatia kuwa mama ana uwezo wa kufanya kazi zaidi ya 3 kwa wakati mmoja ambapo Shirika la (ICS) limeadhimisha kwa kutoa elimu katika Kijiji na Kata ya Bukene Halmashauri ya Wilaya ya Shinyanga.

Baadhi ya Watoto katika Kijiji cha Bukene wakonyesha namna  ya kuwasilisha mawazo yao kwa njia ya Michoro zoezi la elimu limetolewa na Shirika lisilo la kiserikali la ICS 
Watoto wakipewa maelezo namna ya kuwasilisha mawazo yao kwa njia ya michoro toka kwa Mkurugenzi wa ICS Bw. Kudely Sokoine Kijijini Bukene.
Wafanyakazi wa Shirika la ICS wakiendelea kugawa Karatasi na kalamu kwa ajili ya watoto hao kuwasilisha jumbe zao kwa njia ya michoro.
Wafanyakazi wa Shirika la ICS wakiendelea kugawa Karatasi na kalamu kwa ajili ya watoto hao kuwasilisha jumbe zao kwa njia ya michoro
Mkazi wa Kijiji cha Bukene akiwakaribisha viongozi  na wafanyakazi wa ICS Shinyanga.
Kina mama wa Kijiji cha Bukene wakifurahia jambo baada ya kupokea elimu juu ya thamani ya mama pamoja na nafasi ya teknolojia katika familia na malezi.


Watoto wakiendelea na zoezi la uchoraji ili kufikisha jumbe zao kwa wazazi 


Mmoja wa wkazi wa Kijiji cha Bukene akimshukuru shemeji kwa msaada mkubwa aliyompatia wakati mkewe alipojifungua ambapo ameamua kumpa zawadi kama sehemu ya kutambua mchango wake 
Natambua mchngo wako Shemeji yangu wewe ni mama
Natambua Mchago wako Shangazi hakika wewe ni Mama.
Natambua Mchango wako Mke wangu wakati nilipougua kwa muda baada ya kujeruhiwa na Nyoka hakika ulisimama na mimi ongera sana.
Darasa likiendelea kwa watoto 
Meneja Miradi ICS Sabrina Majikata akizungumza na watoto kabla ya kuanza zoezi la uchoraji.
Zoezi la Kugawa vifaa kwa watoto likiendelea
Wafanyakazi wa ICS wakiwa pamoja na baadhi ya kina mama wa kijiji cha Bukene halmashauri ya wilaya ya Shinyanga katika maadhimisho ya siku ya mama duniani
Mchango wako nautambua na kuuthamni ongera wewe ni mama 
Natambua mchango wako Shangazi baada ya baba kuniacha wee ndiyo uliyenifikisha hapa hakika wewe ni mama.
Zoezi la kuandika jumbe za kuonyesha upendo kwa Mke,Mama,Shangazi baada ya kufanyiwa mema muda mwingi kina baba waamua kaundika 

Mkurugenzi wa ICS Bw. Kudely Sokoine akisoma jumbe zilizoandikwa na kina baba kwenda kwa wale wanaowapenda 
Kina mama wakisoma jumbe zilizotumwa kwao kutoka kwa wale wanaowapenda wakiwemo Vijana wao, waume zao  na kaka zao 



Tumechoraaaaaa






Picha ya pamoja kati ya Wafanyakazi wa ICS, wazazi wa  watoto wa kiume na kike kutoka kijiji cha Bukene baada ya kuhitimisha kupokea elimu ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya mama Duniani ambayo ICS imeadhimisha kwa Kutoa elimu Bukene Shinyanga Vijijini.

Post a Comment

0 Comments