Header Ads Widget

MGOMBEA UBUNGE CCM JIMBO LA SOLWA AHMED SALUM ABAINISHA KUENDELEA KUTATUA KERO ZA WANANCHI

Mgombea Ubunge jimbo la Solwa kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ahmed Salum akiwaomba wananchi wamchague tena kuwa Mbunge wa Jimbo la Solwa.

Na Shinyanga Press Club Blog
Mgombea Ubunge jimbo la Solwa kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ahmed Salum anayetetea kiti chake amewaomba wapiga kura wa jimbo hilo wamchague tena kwa kumuongezea  miaka mitano tena ili aendelee kuwaletea maendeleo katika Nyanja mbalimbali ikiwemo sekta ya maji,uchimbaji mdogo na afya.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni katika jimbo hilo zilizofanyika kata ya mwakitolyo Ahmed amesema kuwa anazitambua changamoto na kero mbalimbali  zinazowakabili wananchi wa Solwa ikiwemo miundombinu ya barabara huku akidai kuwa baadhi ya barabara hizo zipo katika utekelezaji wa uboreshaji.

"Kama mnavyofahamu jimbo letu  tunazidi kupambana kutatua kero zinazolikabili ambapo mnafahamu barabara yetu ya Kahama Mwakitolyo hadi Mwanza imekuwa ikikatika mara kwa mara na kukosesha mawasilaiano lakini kwa sasa hali ni tofauti tayari ufumbuzi wa kudumu umeanza kupatikna ikiwemo kujengwa kwa makaravati makubwa"

Ahmed ameendelea kuwaomba wapga kura wa jimbo hilo  wamchague kuwa Mbunge wao pamoja na Rais Magufuli na madiwani wa CCM kwani Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020-2025 inagusa maisha ya Watanzania na CCM imedhamiria kuwaletea maendeleo wananchi huku akigusia suala la wachibaji wadogo

"Kwenu ninyi wakazi wa mwakitolyo mlikuwa mkisumbuliwa sana na utozaji wa kodi ya shilingi laki moja lakini mmesikia maagizo ya Mheshimiwa rais nami nimeshaanza kutekeleza na sasa hiyo kodi haipo wala hakuna usumbufu tena fanyeni kazi zenu kwa amani na usalama zaidi "

Akimnadi Mgombea ubunge wa jimbo hilo Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Shinyanga Mabala Mlolwa amewaomba wananchi kuchagua wagombea wa CCM ili waweze kuwaletea maendeleo yatakayowanufaisha wananchi.

"Niwaombe wana Mwakitolyo na Solwa kwa Ujumla wapigieni kura wagomea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwani ilani inayotekelezwa ni yake na  wanaifahamu vizuri  hivyo itakuwa raisi kutatua na kutekeleza mahitaji yenu"

Naibu Waziri wa Ujenzi ambaye pia ni Mgombea Ubunge aliyepita bila kupigwa katika jimbo la Ushetu wilayani Kahama Elias Kwandikwa amesema Serikali ya CCM inaendelea kuboresha miundombinu ya barabara pamoja na utoaji wa maeneo kwa wachimbaji wadogo wadogo katika eneo la Mwakitolyo hivyo ni muhimu kwa wachimbaji kuchangamkia fursa hiyo. 

"Hali ya eneo la Mwakitolyo pale wakati wa msimu wa mvua palikuwa pakikatika mara kwa mara na kuwapa usumbufu wananchi wanapotakiwa kwenda kupata mahitaji hadi wazunguke kahama na kwenda shinyanga ambapo ni mbali sana sasa ufumbuzi umepatikana kwani serikali imetoa fedha na zoezi la ukwekaji Makaravati makubwa unaendelea"

Kwandikwa ameongeza kuwa serikali ilikuwa ikitoa hilingi milioni 900 kufanya marekebisho ya dharura katika eneo hilo wakati mvua zinapokuwa nyingi na kupelekea kusombwa kwa eneo hilo na wananchi walilazimika kutumia mitumbwi kuvuka kutoka eneo moja hadi jingine 



Kwa upande wake Mjumbe wa NEC, Gaspar Kileo ambaye pia ni Meneja kampeni wa mgombea ubunge jimbo la Shinyanga mjini. Patrobas Katambi amewataka  wapiga kura kuchagua wagombea wa Chama Cha Mapinduzi ili waendelee kutekeleza ilani yao katika kuwaletea maendeleo wananchi wa jimbo la Solwa.

wakimuombea kura mgombea ubunge jimbo la Solwa,Wagombea Ubunge wa viti maalumu Mkoa wa Shinyanga Lucy Mayenga na Santiel Kirumba  wamewaomba wanawake kumpigia kura Dkt. John Pombe Magufuli kuwa Rais wa Tanzania ,Wabunge pamoja na madiwani wa CCM  hali itakayosaidia kuleta maendeleo kwa ushirikiano.

Katika hatua nyingine wagombea hao wamewataka  wachimbaji wadogo kuendelea kuchimba madini ya dhahabu kwa kujiamini bila kubughuziwa wakati serikali ikiendlea kutatua changamoto zao
Mgombea ubunge kwa tiketi ya CCM jimbo la  Solwa akiendelea kunadi sera zake kwa wapiga kura wa jimbo hilo 
 Mgombea Ubunge wa Jimbo la Solwa akiwasili katika uwanja wa Mwakitolyo kwa ajili ya kunadi sera zake 
  Wananchi na wanachama wa CCM wakiwa kwenye uzinduzi wa kampeni za uchaguzi
  Wananchi na wanachama wa CCM wakiwa kwenye uzinduzi wa kampeni za uchaguzi
  Baadhi ya Wagombea wa nafasi ya udiwani kutoka jimbo  la Solwa wakiwa katika picha ya pamoja wakiwa mbele ya wananchi wa Mwakitolyo 
  Mgombea ubunge viti Maalum mkoa wa Shinyanga Dr Christna Mzava  akipiga Magoti akimuombea  kura Rais,Mbunge na Madiwani wa jimbo la Solwa
 Kushoto ni Naibu Waziri wa Ujenzi ambaye ni Mgombea Ubunge aliyepita bila kupigwa katika jimbo la Ushetu Elias Kwandikwa akiwaombea kura wagombea wa CCM. Kulia ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Shinyanga, Mabala Mlolwa
 Mgombea Ubunge jimbo la Solwa kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ahmed Salum akiwa kwenye mkutano wa Uzinduzi wa Kampeni za CCM ambapo amewaomba wananchi wamchague tena kuwa Mbunge wa Jimbo la Solwa.